Friday, November 14, 2014

MCHUNGAJI AFARIKI DUNIA AKIJARIBU KUTEMBEA JUU YA MAJI KAMA YESU


Mchungaji kutoka Nigeria, Frank Kabele (35) amesombwa na maji katika mto mmoja nchini humoo na kufariki alipojaribu kutembea juu ya maji kama Yesu.
 
Frank Kabele aliwaambia waumini wake kuwa mtu mwenye imani anaweza kufanya miujiza yeyote ila tu uwe na imani.
 
Aliwaahidi wafuasi wake kuwa atatembea juu ya maji pindi tu atakapomaliza maombi yake.

Lakini mambo yalienda ndivyo sivyo baada ya mchungaji huyo kujaribu kutembea katika mto mkubwa, alididimia mtoni humo na ilikuwa vigumu kwa waumini wake kumsaidia kwani maji yalikuwa na nguvu nyingi na kufariki dunia.

1 comment:

  1. hahah...kilimsibu nini kutembea juu ya maji wakati hakua na uwezo huo au imani yake iliishia katikati?

    ReplyDelete